Jumamosi 30 Mei 2026 - 14:30
Muqawama haujajikita katika kazi za kijeshi pekee, bali umefunguka hadi katika kulijenga taifa lenye nguvu

Hawza/ Katibu Mkuu wa Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq amesema kuwa; Muqawama haupaswi kutazamwa kuwa umefungika katika shughuli za kijeshi pekee, bali ni mwelekeo unaoendelea kuelekea katika ujenzi wa taifa lenye nguvu na uwezo wa kufanya maamuzi ya kiutawala kwa kujitegemea.

Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Qais Al-Khazali, Katibu Mkuu wa Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq, siku ya Jumatano katika khutba ya Swala ya Idi ya Adh-ha mjini Baghdad, alisema kuwa; Muqawama haupaswi kuwekewa mipaka katika kazi za kijeshi pekee, bali ni mchakato unaoendelea kuelekea katika kulijenga taifa lenye nguvu na uwezo wa kufanya maamuzi ya kiutawala kwa uhuru.

Sheikh Al-Khazali alisema: Kazi ya kijeshi ya Muqawama ilihesabiwa kuwa kipaumbele cha kwanza katika kipindi ambacho serikali ya Iraq ilikuwa inakabiliwa na vitisho.

Alifafanua kwamba; fikra sahihi ya Muqawama inajidhihirisha katika kulijenga taifa lenye nguvu; taifa ambalo lina maamuzi yake ya kujitegemea, mamlaka yake na taasisi zake.

Katibu Mkuu wa Harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq alisisitiza kwamba: Muqawama wowote ambao hauna mradi kamili wa ujenzi, hatua kwa hatua utageuka kuwa mzigo kwa jamii.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha